Beniel Seka
Mtihani wa
kuchagua jibu sahihi una faida na hasara. Baadhi ya wadau, wkiwepo wanachama wa
Chama cha Hisabati Tanzania (MAT/CHAHIA) tayari wameshalalamika kwa viongozi wa
Elimu kuhusu mtihani huo bada ya Baraza la Mitihani la Taifa kuanza kutahini
Hisabati kwa kutumia mtindo huo wa kuchagua jibu sahihi. Aidha baaadhi ya
waliokerwa na jambohili wameshatoa maoni yao kuhusu muundo huu wa kutahini.
Mtihani wa aina hii una madhara mengi ukilinganisha
na faida. Baadhi ya ya hasara ni kuwepo uwezekano wa kubuni majibu
na kuruhusu mazingira ya kuibiana au kupeana majibu. Tayari matokeo ya mtihani wa aina hii
yameshasababisha kizaazaa kwa wanafunzi na walimu wa baadhi ya shule.
Hivi karibuni
tumepata habari kuwa wanafunzi 41 wa Wilaya ya Newala ambao hawajui kusoma na
kuandika wamechaguliwa kujiunga na shule za sekondari. Katika ziara yake wilayani humo, Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais
inayoshughulikia maadili ya viongozi, Kepteni Mstaafu, George Mkuchika,
aligundua kuwa jambo hilo limefanyika katika wilaya hiyo. Alihoji inawezekanaje
mwanafunzi asiyejua kusoma wala kuandika achaguliwe kuingia sekondari.
“Inawezekanaje mwanafunzi akae miaka saba bila kujua kusoma au kuandika halafu akachaguliwa kwenda kidato
cha kwanza! Kwani walimu hawatoi testi wakagundua hilo?”
Akizungumza
kwa lugha kali, Waziri huyo aliwashutumu walimu kwa kuhusika na jambo hilo.
Alisema kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya walimu ambako wanafunzi hao walitoka. “Inawezekana walimu wa shule hizo
walihusika katika tatizo hilo. Lazima wawajibishwe.” Waziri huyo alitoa shutuma hizo alipokuwa anahutubia
wakazi wa wilaya hiyo mwishoni mwa ziara yake.
Akihojiwa na
Nipashe, mmoja wa wazazi wa mwanafunzi aliyechauliwa bila kujua kusoma au
kuandika alisema, “ Mimi najua kuwa mwanangu hajui kusoma wala kuandika.
Kinachonisikitisha ni kwamba nimeshtakiwa kwa kutompeleka mtoto huyo sekondari
baada ya kuchaguliwa. Nimeona hakuna sababu ya kumpeleka mtoto huyo sekondari
kwa kuwa hatafaidi chochote. Hiyo ni kupoteza ada. Hata hivyo bado nasumbuliwa.
“
Katika
mazingira tofauti, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa
Phillip Muluge, akiwa ziarani mkoa wa
Kigoma alifahamishwa kuwepo wanafunzi waliochaguliwa kuingia sekondari wakati hawajui
kusoma wala kuandika. Naibu Waziri huyo
naye aliahidi kuchukuwa hatua kali kwa wahusika. Hivi karibuni hali kama hiyo
imeripotiwa katika wilaya ya Ludewa. Inawezekana kuwa wako wengi ambao bado
hawajatajwa kwa wilaya nyingine na hili kizaazaa na hatari sana kwa Taifa.
Tumekuwa
tunashuhudia katika televisheni zetu tangazo la shirika la Hakielimu likieleza
kuwa wako wanafunzi wengi waliko shule za sekondari ambao hawajui kusoma wala
kuandika. Aidha wanafunzi wengi wameonekana wana mwandikombaya usiowezaa
kusomeka kirahisi. Matatizo haya yameendelea kuwepo kwa kuwa hakuna hatua za
makusudi zinazoelkezwa dhidi yao. Mtihani a kuchagua jibu sahihi umeongeza
ugumu wa tatizo hilo kwa kuwa matokeo yake yanaaminiwa kwa ajili ya uchaguzi
kwenda sekondari bilamchakatowa ziada.
Mwanafunzi aliyemaliza darasa la saba huchaguliwa
kuingia kidato cha kwanza baada ya kufaulu Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi
unaotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa. Baraza hilo lina kiwango cha ufaulu
ambacho mtahiniwa akishapata alama
hiyo (jumla ya maksi zake kwa
masomo yote) au kukivuka, huhesabiwa amefaulu. Kwa mujibu wa sera ya serikali,
mwanafunzi anayefaulu anastahili kwenda shule ya sekondari. Hatujasikia sera
tofauti.
Mtihani huo
unaofanywa mwishoni mwa darasa la saba ni wa kchagua wanafunzi kungia sekondari
na si wa ufanisi. Mtihani huo hauna cheti. Cheti cha kumaliza elimu ya msingi
kinatolewa kwa utaratibu mwingine. Kwa hiyo, mtihani unakuwa umemaliza kazi iliyotakiwa
baada ya kutoa matkeo. Kinachobakia ni kuchagua wanafunzi kuingia shule
mbalimbali zikiwepo za vipaji maalumu.
Mtihani huo
wa Baraza hutumia muundo wa maswali ya kuchagua jibu sahihi. Tumekwishaona madhara
ya mtihani huo hasa kwa madarasa ya chini. Mtihani wa aina hiyo unafaa zaidi
kwa watu waliokomaa ili watumie muda wao kuchambua majibu. Mwanafuzi anaweza
kuvuka kiwango cha ufaulu kwa kubuni au
kwa kuibia. Kama vigezo vingine havitatumika , basi mwanafunzi ana kila sababu
ya kutumia mwanya huo kwenda sekondari.
Mawaziri wetu wameahidi kuchukuwa hatua kali
kwa wahusika. Hilo ni jambo zuri lakini linapaswa kufanyika kwa uangalifu. Sina
uhakika kama kuna sera inayomkataza mwanafunzi kutofanya mtihani huo kama hajui
kusoma wala kuandika. Kama ipo, mwalimu mkuu na wahusika wengine wana hatia. Kama
haipo, inafaa kuiingiza ili tatizo hili lisitokee tena. Mwanafunzi asiyejua
kusoma au kuandikwa hapaswi kufanya huo mtihani.
Katika ngazi
ya sekondari, Baraza la Mitihani la Taifa hutoa mtihani wa “maarifa” (Qualifying Test) kwa watahiniwa
binafsi (wale wasiokuwa kwenye shule za sekondari zilizosajiliwa). Lengo ni
kuhakikisha kwamba kabla ya kufanya mtihani wa kitaifa wa kumaliza sekondari na
kutunukiwa cheti, mtahiniwa awe amefikia kiwango cha kuridhisha cha elimu hiyo.
Wale wanaoshindwa kufaulu mtihani huo hawaruhusiwi kufanya mtihani huo wa
cheti. Chuo Kikuu mwanafunzi haruhusiwi kufanya mtihani ikiwa itathibitishwa
hajahudhuria idadi kadhaa ya mihadhara.
Kuna
uwezekano pia walimu wasio na uaminifu au watoto wa sekondari, kumrubuni
msimamizi kuwaandikia wanafunzi hao majibu kwa kuwa ni rahisi kuyanakili. Kama
mtihani ungekuwa na maswali ya kujieleza ingewawia vigumu kufanya hivyo. Kabla
ya mtihani wa Hisabati kutumia mtindo huo tulikuwa tunashuhudia wanfunzi hao
wasiojua kusoma wala kuandika wakipata sifuri. Hilo limepungua sana katika mtihani
wa mwaka jana (2011).
Jambo
jingine la kuzingatia ni mkazo ambao mtihani huo unapewa. Bado kuna watu wengi
ambao wanafanya kila wanaloweza ili watoto wao waingie sekondari. Pia viongozi
wa wilaya ambazo shule zao hufanya vibaya katika mtihani huo huwajibishwa. Hofu
hii huweza kuwaingiza baadhi yao kushiriki katika mbinu chafu za kupata matokeo
mazuri. Vilevile shule ambazo hupeleka wanafunzi wengi sekondari huonekana bora
zaidi ya zile zinazopeleka wachache.
Athari
nyingine ambayo inaweza kulikumba Taifa ni walimu kupunguza ari ya kujifunza na
wanafunzi pia kutomakinika katika kujifunza wakielewa kuwa mtihani ni wa
kuchagua majibu. Hivi umewahi kufikiria kwamba ukimpa mwanafuzi wa darasa la
nne anaweza kufanya vizuri hata kumpita wa darasa la saba, mradi tu aweke alama
kwenye visanduku husika? Itakuwa balaa.
Kama nilivyoeleza
mwanzoni mwa makala haya, mtihani wa kuchagua jibu unaweza kusababisha kizaazaa na kufunika zile sifa za muundo
huo wa mtihani. Waziri Mkuchika alipouliza kwamba wanafunzi hao walikuwa
hawafanyi testi au kuandika matini (notes), alikuwa ameleta hoja nzuri. Sisi
tunahoji kwamba ni lazima mtihani huo
uwepo ukizingatia gharama za kuuendesha na kuchakata matokeo? Lazima tukubali
kubadilika.
End
(Mwananchi)
No comments:
Post a Comment