Hivi karibuni mnunuzi
wa vitabu alinipigia simu. Alinipigia kwa kuwa alijua nimeandika
vitabu vingi vya watoto . Aliniuliza kama
nimesikia kwmba kuna tamasha la vitabu mwezi Novemba,
2012.
Nilimjibu kuwa sikuwa na habari. Huenda walikuweko wengine waliokuwa kama mimi. Nilifuatilia na kupata habari kuwa kulikuwa na
mpango huo na tamasha hilo lilikuwa lifanyike
huko Ubungo Plaza,
Dar es Salaam.
Hatimaye tamasha lilifanyika Blue Pearl, hapo Ubungo Plaza
kuanzia tarehe 25 Novemba ambapo wahudhuriaji wengi walikuwa wanafunzi.
Miaka michache
iliyopita mradi wa watoto Tanzania
ulifanya kozi ya waandishi wa vitabu vya aina hiyo katika Chuo cha Ualimu Marangu.Siku
moja wakati mkufunzi anaendelea kutoa mada kuhusu lugha katika vitabu vya watoto,
ilisikika sauti ya mlango kugongwa kwa nje. Alitazama huku na kule lakini
hakuona mtu aliyegonga mlango. Alirejea kwenye ukumbi na kuendelea na mada yake.
Dakika chache baadaye
mlango uligongwa tena. Mimi nikiwa msikilizaji nilikerwa na huo ukatishaji wa
mada. Nilitoka ghafla kabla mtoa mada hajaamua kwenda mlangoni.Yeye aliendelea
kufundisha baada ya mimi kumsaidia. Nilifungua mlango, nami vilevile
sikumuona aliyegonga mlango. Nilitoka nje kabisa na kutazama pande zote. Kwa
mbali niliweza kumwona mototo mmoja amejificha nikamwita, “njoo hapa mtoto.” Aliondoka
na kuanza kukimbia. Kumbe kulikuwepo na wenzie wapatao
kumi.
Wakiungana na wenzie
kukimbia walitamka kwa nguvu, “Tunaomba vitabu. Tunaomba vitabu.”
Sauti hiyo iliwafikia hata wale waliokua wanamsikiliza mtoa mada. Niliporudi
kwenye ukumbi niliwaarifu kuhusu hiyo rai ambayo iliwagusa wengi.
Mratibu wa kozi
alikiri kuwa jana yake, watoto kadhaa wa
Shule ya Mazoezi walitembelea eneo la ukumbi huo na kuuliza maswali kadhaa
kuhusu miswada iliyokua ikijadiliwa. Mratibu aliwapa zawadi ya vitabu baada ya kuonyesha shauku kubwa ya
kusoma vitabu. Hii ikawa kichocheo kikubwa kwa watoto wengine kujitokeza kusoma
vitabu.
Hapo hapo nilikumbuka
Siku ya Kitabu kwa Watoto (Children’s Book Day) iliyoyosherekewa kwenye ukumbi
wa Makumbusho yaTaifa
(National
Museum). Profesa Penina Mlama alikuwa mgeni rasmi wa
heshima mwaka 1993. Profesa Mlama akishirikiana na Profesa
Lihamba wa Chuo Kikuu cha Dsm, aliwafundisha
watoto wimbo ufuatao:
Baba yangu naomba kitabu ; kimoja tu tafadhali
Mama yangu naomba kitabu; kimoja tu tafadhali
Kaka yangu naomba kitabu; kimoja tu tafadhali
Dada yangu naomba kitabu; kimoja tu tafadhali
Mjomba yangu naomba kitabu; kimoja tu Tafadhali
Shangazi yangu naomba kitabu; kimoja tu Tafadhali.
Waliimba wimbo kwa
furaha na matumaini. Kila ninapoona kitabu kipya huwa nawakumbuka sana watoto. Wana
hamu na kitabu. Je, watakiona? Je, kuna hata mtu wa kuwaambia
kipo? Hawa wanaoshiriki ni wale wachache tu walioalikwa.
Wengine, je? Tuwaambie na tuwapatie vitabu.Watoto wana hamu ya kusoma vitabu lakini
hawavipati.
Kila mwaka ifikapo
mwezi Septemba
hufanyika tamasha la vitabu.Tamasha la mwaka huu limecheleweshwa hadi Novemba.
Bila shaka kulikuwa na sababu za kufanya hivyo. Tunashukuru kwamba limekuwepo. Kama
ambavyo vyombo vya habari vilivyoripoti
pamoja na uzuri wa tamasha lenyewe ni watu wachache sana waliolijua. Kwa jumla,
watu wengi hawakujua kuwa kulikua na shughuli muhimu namna hiyo hapa Dar es
salaam.Tamasha hilo
lilifanyika mikoa mingine pia.
Kwa mara nyingine,mradi
wa vitabu vya watoto (Children’s Book Project) umeandaa wiki ya usomaji ya
usomaji ambayo inafikia kilele chake jumamosi tarehe 9/11/2010.Wiki hiyo
imeshuhudia mashindano ya usomaji ,uchoraji,kutumia kamusi,chemsha bongo na
utungaji wa hadithi kwa shule zilizopo katika programu ya usomaji zilizopo
mikoa ya pwani na Dar es salaam. Aidha shule zimeshindanishwa kwenye
matumizi ya uendeshaji wa maktaba na utengenezaji wa zana za kujifunzia na
kufundishia.
Shughuli hizi zinafikia
kilele chake katika shule ya uhuru wasichana iliyopo maeneo ya manispaa ya Ilala
ambapo washindi mbalimbaliwatapewa zawadi.Kutakua na maonyesho mbalimbali ya uhamasishaji wa usomaji. Aidha
wachapishaji
watakuwepo kuonyesha na kukuza vitabu kwa wale watakaohitaji huduma
hiyo.Shughuli hii ni wazi kwa umma.Wazazi wa watoto walioshinda kwenye
mashindano hayo wameshauriwa wawepo kwenye sherehe hiyo kuwaunga mkono watoto
wao.
Mimi nimeona kwamba
nizisambaze habari hizi baada ya kudokezwa.Tunalo jukumu kubwa la kukuza tabia
ya usomaji. Njoo tukaone wametuandikia nini. Mimi
nitakuwepo je, wewe?
Hivi karibuni gazeti
la nipashe lilichapisha makala iliyohoji kuna uhaba wa vitabu.Makala hiyo
ilielezea kuwa uhaba huo sasa ni wa kufikirika tu maana vitabu vimejaa kwenye
ghala na maduka ya wauzaji vitabu.Tatizo ni kwamba havinunuliwi kwa sababu
mbalimbali, mojawapo ya sababu ni ubinafsi
uliokithiri kwa baadhi ya wale wenye dhamana ya kununua vitabu.
Vilevile umma umekua
na muamko finyu wa kusoma vitabu. Ni mara chache sana utaona watu wanasoma
vitabu majumbani mwao, sehemu za mapumziko na hata
kwenye vyombo vya usafiri. Hii ni tofauti na wenzetu kutoka nchi
za nje ambao
hubeba vitabu vidogo na vikubwa kila waendapo. Kila wanapopata
mwanya hutumia nafasi hiyo kujisomea. Hata usomaji wa magazeti nao
unalegalega. Ukiona kikundi cha watu wanasoma, utagundua kuwa wengi wao wansoma
habari za michezo hasa mpira wa miguu na mambo ya udaku.
Mara nyingi ninapowaambia
watu wanunue vitabu husema kuwa hawana watoto. Wanadhani
vitabu ni vya watoto tu. Vitabu vya kujisomea ndio havinunuliwi kabisa. Utasikia
mtu akisema baada ya kukitazama kitabu , “Hiki
ni cha darasa la ngapi?” Wanauliza zaidi vitabu vya kiada na
kama ndicho wanachotumia darasani.
Siku za karibuni TBC1 ilimhoji Mama
Truphina Nsemwa wa Maktaba Kuu ya Taifa ambaye alilalamika kuhusu hali duni ya
usomaji wa vitabu hapa nchini. “Ni watoto wachache tu
wanafika maktaba kwa ajili ya kujisomea. Wengi wanaotumia maktaba zetu ni wale
wanaojiandaa kwa mitihani tu.” Nayo BBC, London walikiri kuwa walipotembelea
maktaba hiyo ya taifa walikuta watoto tu wanajisomea. Hawakuwepo watu wazima.
Kwa namana hiyo tutafika tulikokusudia?
No comments:
Post a Comment