NA BENIEL SEKA
Somo
la Hisabati limeendelea kuwa somo linalowatesa wengi. Hali ya wanafunzi kuliogopa
somo hilo na kuendelea kufanya vibaya imeendelea. Tufanye nini? Hebu kwanza
tuangalie simulizi hii.
Siku
moja msichana aitwaye Eva na rafiki yake aitwaye Roda walikuwa wanaongea.
Mwalimu mmoja aitwaye Vesika aliwakuta na kuwasalimu. Wote wawili walikuwa
wanamjua Mwalimu Vesika kuwa ni mtaalamu wa Hisabati. Walionekana kumfurahia
kwa namna walivyomsalimia kwa uchangamfu.
Baada
ya salamu, Eva alimuuliza, “Hivi mwalimu naweza nikajua Hisabati?”
Mwalimu
Vesika alimtazama kwa shauku ya kujua kulikoni. “Kwa nini usiweze? Kwani
Hisabati imekufanyaje?” alimuuliza kwa huruma.
“Nimeliona
kuwa ni somo gumu. Nilipokuwa shuleni sikuwahi kulipenda. Hata mwalimu nilikuwa
simpendi maana alikuwa ananigombeza nilipokosea. Matokeo yake sikujiamini hata
kidogo nilipokuwa nafanya mtihani.”
Roda
aliyekuwa anamsikiliza mwenzake kwa makini aliongeza, “Mimi niliachana nalo
nilipokuwa kidato cha pili tu. ‘Majometri’ yake na ‘makongruensi’ yake
yaliniweka mahali pabaya. Nilifeli Hisabati kidato cha nne na hadi sasa
sijalitafutia dawa. Kwa sasa nasikia kuna kazi ya kujiendeleza lakini inahitaji
Hisabati. Sijui nitaimudu vipi.”
Mwalimu
Vesika aliwatazama kwa huruma huku akikuna kichwa. “Itabidi mbadilishe msimamo
wenu kuhusu Hisabati. Lazima mjenge urafiki na Hisabati. Somo la Hisabati si
gumu kama baadhi ya watu wanavyodai. Kama ungekuwa umefuatilia mtaalamu mmoja
wa Hisabati akielezea katika redio, televisheni na magazeti kuhusu kauli hiyo
potofu, ungekuwa umeanza kuchukua hatua.”
Hapo
Eva hakujizuia kutamka, “Kwa wale wanaoziweza wanasema si ngumu. Sisi ndio
tunaopambana nalo, ndio tunauona ugumu wake. Naomba uniambie siri ya
kufanikiwa?
“Hakuna
siri. Ni suala la kulipenda, kusikiliza na kutii maelekezo na kufanya mazoezi
mengi. Kwa kufanya mazoezi mengi utapenda kusoma vitabu mbalimbali ambavyo
vitazidi kupanua uwezo wako wa kufikiri na kubuni njia mbadala za kufumbua
matatizo. Wakati mwingine unaweza kumzidi hata mwalimu wako. Kumbuka, ulimwengu
wa sasa una mitandao yenye taaluma nyingi. Unaweza kujikuta unaenda sanjari na utandawazi.
Unasemaje, Eva?”
Eva
alisema, “Mwalimu hapo unatuvika vilemba vya ukoka. Mtu kama mimi niwe mtaalamu
wa Hisabati. Hata intaneti inikome! Si itakuwa moja ya maajabu ya dunia, kitu
ambacho hata mlima Kilimanjaro pamoja na umaarufu wake haukuweza kupewa!”
“Hapana,”
Mwalimu Vesika alimkatalia, “Haitachukuwa muda mfupi, lakini inawezekana.
Katika historia ya binadamu, wako watu walioanza kwa hali duni lakini kwa
kujitahidi wakaweza kufanya mambo makubwa na kuishangaza dunia. Hata nyie
mnaweza. Unajua mimi nilipokuwa darasa la kwanza niliwahi kurudishwa nyumbani
inende na mzazikwa kuwa nilikuwa sina maendeleo mazuri katika somo la Hisabati.
Mtaa mzima ulijua jambohilo. Nilifedheheka sana.”
“Ikawaje?” Eva aliuliza kwa shauku.
“Kutofanya
bidii kwangu kulitokana na mwalimu wangu kunipiga sana nilipokosea Hesabu. Hii ilinisababisha
niwe mtoro. Hali ikazidikuwa mbaya.” Mwalimu Vesika alifafanua. “Ilibidi
nibadilike. Nilianza kujitahidi na nilipofika darasa la nne, tayari nilikuwa
nafanya vizuri kuliko baadhi ya wenzangu. Nilipofika darasa la sita nilianza
kuwa tishio kwa wenzangu baada ya kuwa wa kwanza darasani kwenye mtihani wa
muhula katika somo la Hesabu.”
Mara
mvulana mmoja aitwaye Mika akajiunga nao. Aliwasikiliza na kusema “Mnaongelea
Hisabati? Mimi kwa sasa hainipi taabu. Mwanzoni ilikuwa kasheshe. Kuna siku
mwalimu alisema, “nusu mara nusu” ni “robo”. Nilishanga na kusema tangu lini
ukazidisha kitu kikapungua? Ukizidisha unatakiwa kupata namba kubwa zaidi. Nusu
ni kubwa kuliko robo, Hapo nilianza kufikiri hisabati inadanganya.”
Roda
alidakia na kusema, “Ulibadilika lini?”
“Sikubadilika
kwa muda mrefu. Nilianza utundu. Walimu walibidi wanivumilie, la sivyo
ningeishia pabaya. Hatimaye waliniita Ziro,
maana nilikuwa natoa majibu yasiyokubalika, yenye uchizi. Siku moja mwalimu
wetu aliuliza ‘nane gawanya kwa mbili unapata nini?’ Mimi nilijibu, ‘inategemea
umegawanyaje? Kwa wima au kwa ulalo?” Wanafunzi wote darasani walicheka. Wao
walijua jibu ni rahisi yaani nne. Walimshngaa ‘Ziro’ alivyokuwa anamsumbua
mwalimu. “Una maana gani kugawanya kwa wima?” Mwalimu alimtaka atoe maelezo.
“Nilikwenda
ubaoni na kukata mstari katikati ya tarakimu hiyo 8. Kwa ulalo unapata sifuri
mbili. Kwa wima unapata tatu mbili zilizogeukiana nilieleza. Tangu wakati huo
walimu wakaanza kuuliza maswali kwa uangalifu. Hii ilinifanya nitumie mantiki
kukabiliana na changamoto za hisabati. Nikawa nalifurahia somo.”
“
Kwa kweli kuna njia nyingi za kulipenda somo. Wengine mpaka muitwe ziro. Hii
nitaisimulia popote,”
alisema Eva huku akicheka.
“Njia
pekee ni kuongeza kujiamini. Hisabati hufuata mantiki. Ukishaielewa dhana ni
rahisi kujijengea kanuni mbalimbali zinazohusiana nazo. Vilevile unaweza
kugundua njia mbadala za kufumbua matatizo. Pengine njia utakayogundua ikawa
rahisi kuliko zile ulizojifunza. Utajisikia mwenye furaha sana.”
“Ni
kweli kabisa, mwalimu.” Yule mvulana alikubaliana naye. “Nilipoelewa maana ya
pai, kwa mfano, niliweza kuunda mwenyewe kanuni ya kukokotoa mzingo wa duara
(mduara) kwa kuzidisha pai mara kipenyo. Baadaye nilikuja kuikuta kwenye
kitabu. Hii iliniongezea kujiamini.”
Kama ulivyoshuhudia mazungumzo hayo, upenzi wa
somo la Hisabati ndio nguzo kuu ya kulimudu somo hilo. Ukifanya mazoezi mengi
utaweza kugundua njia mbalimbai za kukabiliana na ugumu wa somo hilo na hapo
hapo ukawa mgunduzi. Unangoja nini? Chukua hatua sasa.
Kisha
aliendelea kusema, “Kitu cha ziada cha kufanya ni kuhudhuria kongamano,
midahalo au semina mbalimbali za Hisabati. Ni muhimu kuzitafuta ili ufaidike na
mawazo yatakayotolewa na wataalamu. Kwa mfano, chama cha Hisabati cha Tanzania
(MAT/CHAHITA) kilifanya semina ya Hisabati huko Chuo Kikuu cha Tumaini tawi la
Iringa kuanzia 12 Septemba hadi 17 Septemba 2011. Je, ulibahatika kuhudhuria?
Mwaka jana iliafanyka tarehe 17 Septemba hadi 22Septemba katika
Chuo cha Makumira, Arusha. Mwaka huu inafanyiha Mbeya mwezi huo huo wa September. Ni vyema basi ukafanya jitihada ya kutafuta ufadhili
ili uhudhurie. Kazi kwako.
No comments:
Post a Comment